Saturday, November 25, 2006

KARIBUNI BONGO CELEBRITY

Karibuni katika Bongo Celebrity.Hii ni blog ambayo itakuwa inaandika kuhusu watu mashuhuri wa Tanzania na pia Afrika Mashariki.Tupende,tusipende maisha ya watu mashuhuri/maarufu(celebrities) yana mvuto mkubwa kwa jamii yetu.Iwe ni mwanasiasa,mwanamuziki,msakata kabumbu, mchekeshaji,mcheza sinema,mpiga simu maarufu redioni,msanii wa ngoma za asili,za kisasa,mtangazaji maarufu wa tv au redio,mtu mwenye umbo la aina yake nk nk wote kwa pamoja ndio huwa vivutio katika jamii. Blog hii itajikita katika kuandika habari za watu hao maarufu.

Pia blog hii inatarajia kuwa ndio chanzo cha habari mpya,chanzo cha matoleo mapya ya albamu za muziki,habari za chochote kile kipya ndani ya jamii zetu nk.Karibuni sana.